Old school Swatch Watches



THIS PAGE IS PROUDLY SPONSORED BY NASSOR JANGWA, Karibu katika ukurasa huu. Unakaribishwa kutoa maoni yako yoyote yatakayo jenga. Nawasihi kilammoja wetu ajiheshimu kwa kutumia lugha zisizochafua hali ya hewa. Yaliyomo humu sijamlenga yoyote kwa ubaya,toa maoni au ushauri pale chini na si vinginevyo. Akhsanteni!
KIZAAZAA CHA MCHINA
TAIFA LINAPITIA KIPINDI KIGUMU
Na Mwandishi Wetu TAIFA linapita katika kipindi kigumu, mtafaruku wa sakata la Katiba Mpya, ufisadi Wizara ya Nishati na Madini, tishio la kujichomeka nchini kundi hatari la Wasomali, Al Shabaab, migogoro ya wanafunzi, wamachinga, ardhi na mengine yote lakini yanabaki nusu shari. Shari kamili ni ujumbe mkali kutoka kwa waasi uliotumwakwa viongozi wa nchi, wakiwataka kuachia madaraka ndani ya siku 100, vinginevyo watawaondoa kwa nguvu. Habari za ndani zinasema kuwa ujumbe huo hatari, umetumwa kupitia waraka pepe na SMS kwenda kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete,wakimpa siku 100 awe ameachia madaraka, vinginevyo wahusika watatumia nguvu. Ujumbe huo, umeelekezwa pia kwa Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha amesema kuwa serikali inafanya uchunguzi kuweza kuwabaini wahusika na kuwataka wananchi watoe ushirikiano. Imeelezwa kuwa waraka huo umetumwa na kiongozi wa kikundi cha watu 2,858 ambacho kimejitambulisha kwamba kinatokana na muungano wa askari waajiriwa kutoka majeshi mawili nchini. Katika madai yao ya msingi, kikundi hicho kinadai kuwa viongozi waliopo madarakani wameshindwa kazi ya kuongoza nchi, hivyo wamewapa siku 100 waondoke, vinginevyo watatumia nguvu kuwaondoa. “Jeshi la polisi limeanza kufanya uchunguzi kubaini watu hao na wakipatikana tuanze kuwahoji ili hatua zichukuliwe,” alisema Nahodha. Nakala ya waraka huo wa vitisho ulitumwa pia kwa Jeshi la Polisi Tanzania, Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Idara ya Usalama wa Taifa Makao Makuu, Wizara ya Mambo ya Nje, Benki Kuu ya Tanzania (BOT) na ubalozi wa Marekani Tanzania. Nakala nyingine zimetumwa kwa Kamanda Mkuu wa Al Shabaab, ubalozi wa Uingereza Tanzania, Umoja wa Mataifa (UN), Umoja wa Afrika (AU), mashirika yasiyo ya kiserikali ya ndani na nje ya Tanzania pamoja na vyombo vya habari. HOFU YATANDA Wakati vitisho hivyo vinatokea, kikundi cha Al Shabaab kinachotikisa nchi za Somalia na Kenya, kinatajwa kuweka kambi Dar es Salaam na kuendesha mafunzo ya ugaidi ili kuandaa mapambano ya kile wanachokiita Jihad ya kuihami Dini ya Kiislam. Tayari jeshi la polisi nchini linawashikilia watu kadhaa wanaojihusisha kwa namna mbalimbali na harakati za Al Shabaab. Sakata la Katiba Mpya nalo ni kizungumkuti, kwani kwa sura pana, linaelekea kuipeleka nchi kwenye machafuko. Tayari viongozi kadhaa wa serikali wameshatoa tuhuma kwamba kuna matajiri wanaomwaga fedha ili kufadhili vurugu mbalimbali zinazochagizwa na migomo, maandamano na kadhalika. Rais Kikwete, alipohutubia taifa mwishoni mwa wiki iliyopita kupitia wazee wa Dar es Salaam alisema, kuna watu hawaitakii mema nchi ndiyo maana hata dhamira njema ya kuihuisha katiba, wanaikataa na kutaka kuitisha maandamano. “Walisema Uchaguzi Mkuu 2015 bila Katiba Mpya patakuwa hapatoshi, sasa tunataka patoshe bado matatizo, jamani uongozi ni kazi kweli,” alisema JK. Hotuba hiyo ya JK, inafuatia kauli mbalimbali za baadhi ya viongozi wa kisiasa na wanaharakati waliotoa tamko kuwa endapo muswada wa kuundwa kamati ya kusimamia maoni ya wananchi kuhusu utunzi wa katiba, itapishwa na bunge, wataingia mtaani kudai haki kwa maandamano. Ijumaa iliyopita, bunge lilipitisha muswada huo, hivyo kuufanya kuwa sheria. Wakati ghasia hizo zikiendelea, serikali inapitia kipindi kigumu kutokana na kitimtimu cha Wizara ya Nishati na Madini, kilichoanzia kama skendo ya rushwa kwenye Bunge la Bajeti la mwaka 2011-2012, ikimgonga aliyekuwa katibu mkuu wa wizara hiyo, David Jairo. Kutokana na jitihada za Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG), Ludovick Utouh kumsafisha Jairo na skendo ya kukusanya shilingi bilioni moja ili kuwahonga wabunge waweze kupitisha bajeti ya wizara yake, Jumamosi iliyopita yaliibuka makubwa zaidi. Kamati Teule ya Bunge, ilisoma ripoti yake na kueleza kubaini ufisadi wa fedha za serikali, hivyo kutoa mapendekezo kwamba Jairo, Luhanjo, Utouh na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja wachukuliwe hatua zinazofaa. Ilibainishwa ndani ya ripoti kuwa kuna skendo ya kughushi fedha iliyofanywa na Jairo kwa kuandika kiasi kikubwa kuliko malipo yaliyofanyika, jambo ambalo ni kosa la jinai. Baada ya ripoti hiyo, wabunge walikuja juu kwa kutaka wahusika wafukuzwe na wafikishwe mahakamani na kubainisha kwamba uozo huo ni sehemu ya ufisadi wa mabilioni ya shilingi yanayokwapuliwa kila kukicha serikalini. Katika ripoti ya Kamati Teule ya Bunge, Jairo alikutwa na hatia ya kukusanya fedha kinyume cha utaratibu pamoja na udanganyifu wa malipo. Skendo hiyo iliibuliwa na Mbunge wa Kilindi (CCM), BeatriceShelukindo aliyesoma bungeni barua ya Jairo kwenda kwa wakuu wa idara zilizo chini ya Wizara ya Nishati na Madini,akielekeza kila moja itoe mchango wa shilingi milioni 50 ili kurahisisha kupita kwa bajeti ya wizara hiyo. Ikaelezwa kuwa idara 20 zilichangia, hivyo kufanya zipatikane jumla ya shilingi bilioni moja ambazo inadaiwa lilikuwa ni fungu la kutoa rushwa kwa wabunge ili wapitishe bajeti ya wizara hiyo.
TABIA ZA WATU.
Nose cleansing
Nose cleansing

Usafi wa masikio unatakiwa uufanye bafuni ukiwa unaoga ama chumbani unavaa peke yako au na mtu wako wa karibu zaidi, sio mbele za watu bila kujali mazingira uliyopo, HAIPENDEZI. Tabia nyingine mbaya ni hii, Utakuta mtu anachokonoapua mpaka unayemuona unajisikia vibaya, au unamuongelesha yeye yuko na pua sijui ni kutojiamini au ni vipi. Ebu hona huyu naye, watuwengine midomo inanuka lakini wamekalia kujichokonoa tu ..................
MAADILI;
Bestiality: Girl Dumps Boyfriend and Horse on Video
Bestiality: Girl Dumps Boyfriend and Horse on Video

Kuporomoka Kwa Maadili, Kushamiri Kwa Ushoga Na Ukahaba Katika zama zetu za leo kuna janga kubwa linalohatarisha uhai wa jamii ulimwenguni. Mithili ya virusi vinavyoua mwili, janga hili linasababisha msiba mkubwa wa kijamii. Janga hilo ni mmomonyoko wa maadili ambayo husaidia kustawisha jamii ya Ushoga, Ukahaba na uhusiano haramuwa kijinsia kabla ya ndoa na nje ya ndoa, Filamu za ngono, Picha za ngono, unyanyasaji wa kijinsia na ongezeko la maradhi ya zinaa, mashindano ya kukaa uchi maarufu ulimbwende, uuzaji na utumiaji wa vileo na dawa za kulevya miongoni mwa vijana ni miongoni mwa ishara kubwa za kuporomoka kwa maadili. Ushoga, usagaji, ubasha na ukahaba ni jambo baya na lisilokubalika kwenye jamii iliostaarabika, na karibia dini zote jambo ili linachukuliwa kuwa ni dhambi kubwa sana. Binadamu hapaswi kufuata mwendo huu ambao ni kinyume na maumbile aloumbiwa. Mambo haya ndiyo yamekuwa yakizishughulisha jamii. Idadi kubwa ya watu haijali hatari hii inayozidi kuwa kubwa na wanaiona kama jambo la kawaida tu. Lakini takwimu zinaonesha kuwa kila siku ipitayo kiwango cha hatari kinazidi kuongezeka. Ongezeko la maradhi ya zinaa ni kigezo kikuu cha kusaidia kuonesha ukubwa wa matatizo yanayomkabili mwanadamu. Kwa mujibu wa rekodi za Shirika la Afya ulimwenguni magonjwa yanayotokana na zinaa yanachukuwa sehemu kubwa ya maradhi. Ripoti zinaonesha kuwa kati ya kesi mpya za magonjwa ya zinaa zinazokadiriwa kufikia milioni 333 kila mwaka ulimwenguni kote, Ukimwi ndio tatizo kubwa zaidi. Kuna ongezeko la idadi ya maambukizi ya ukimwi yanayofikia watu million 2.6 kila mwaka, na vifo vya watu visivyopungua milioni 1.8 kwa mwaka. Takwimu za Shirika la Afya ulimwenguni (WHO) zinaonesha kuwa idadi ya vifo vinavyotokana na ugonjwa wa Ukimwi tokea pale ulipoanza imefikia watu milioni 18.8. Ripoti za shirika hilo kwa mwaka 2000 zinaielezea hivi hali ya mambo: “ Ukimwi una nafasi ya kipekee katika kuleta athari mbaya za kijamii, kiuchumi na katika mipango ya sensa ya maendeleo ”. Miongoni mwa mambo mabaya kabisa yanayozidi kushamiri ni ushoga. Katika baadhi ya nchi jambo hili limehalalishwa kama ndoa, linapewa heshima zote za ndoa na limeundiwa vyama na jumuiya. Duniani kote uovu huu unapingwa. Kushamiri kwa ushoga hivi leo kunatukumbusha hatima ya watu wa Lut waliokithiri katika uovu huu. Kama isemavyo Qur’an na Biblia, walipoukataa wito wa Lut kuiendea njia sahihi, Mwenyezi Mungu aliuangamiza mji na watu wake kwa maangamizi makubwa. Ushoga wa aina yoyote ule ni Haramu kwa mujibu wa Qur\'an na Biblia kwa kupitia mifano ya Kaumu Lut. Aya zifuatazo zinatufahamisha wazi kuwa Ushoga kwa jinsi yake umekatazwa kwa binadamu wote. Na tulimtuma Lut\', alipo waambia watu wake: Je, mnafanya uchafu ambao hajakutangulieni yeyote kwa uchafu huo katika viumbe vyote! Hivyo nyinyi mnawaingilia wanaume kwa matamanio mkwawacha wanawake? Kumbe nyinyi ni watu wafujaji! Q 80-81 Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo. Leviticus 18:22 \"J e! Katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume? Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnao ruka mipaka! \" Q 26:165-166 Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti... 1 Corinthians 6:9 Mwenyezi Mungu amekataza mahusiano yoyote yale kati ya Mume na Mke, nje ya ndoa au mahusiano ya jinsia moja yaani wanaume kwa wanaume au wanawake kwa wanawake. Mashoga wengi wakisaidiwa na wanasiasa, madaktari na wanaharakati kama vile TGNP (Tanzania Gender Networking Programme) uona ushoga kama hali ya kuzaliwa nao na ni uhuru wa mtu kuchagua aina ya maishayake na jinsi ya kuyaendesha. Madaktari wenye kushabikia hali hii ya ushoga, usema kuwa wengi wao mashoga wamezaliwa wakiwa na gene za ushoga kwa hali hiyo hawapaswi kwenda kinyume na matashi na matakwa ya nafsi zao kwa kuwa wameumbwa au kuzaliwa hivyo. Swali la kuwauliza ni ili vipi wale wenye tabia ya wizi, ubakaji na uuwaji, je nao wamerithi au wamezaliwa na jene za tabia hizo za wizi na ubakaji!? Je wale wanao waingilia wanyama (bestiality) na wanaotembea na watoto zao wa kuwazaa (incest), vipi nao wamezaliwa hivyo!? Je madaktari wanatufahamisha nini kuhusianan na swala hili la kuzaliwa na gene zinazodaiwa kuwa zinasababisha ushoga?
HABARI KATIKA MAGAZETI YETU YA NDANI YA NCHI
HABARI LEO
RISASI
UWAZI
IJUMAA
MWANANCHI
HABARI ZA KIMATAIFA NA VYANZO VYA HABARI.
ARTISTdirect.com

World - Google News

Top Stories - Google News

Hollywood.com - Recent News

Sports - Google News

Business - Google News

Sci/Tech - Google News


MARADHI YANAYOMSIBU BINAADAMU NA TIBA YAKE A.MATATIZO YA MZIO (ALLERGY). MATATIZO mengi kuhusu maradhi katika mfumo wa kupumua hutokana na hisia kali sana dhidi ya baadhi ya vitu.Vitu hivi baadae humsababishia madhara maarufu kwa jina la Allergy. Mfano wa vitu hivi ni: pamoja na baadhi ya vyakula; Kufisidika au kuharibika kwa maji(water pollution); Kufisidika au kuchafuka kwa hewa, kwa mfano vumbi(air pollution);Mabadiliko ya hali ya anga au hewa na mabadiliko ya hali ya misimu; Kemikali, gesi, harufu mbaya au uvundo, moshi; Dawa za kumeza. Mafuta mazuri, hata harufu ya vipodozi au manukato; Na baadhi ya vitu vingine, ambavyo mtu havipendi na pengine humdhuru. Vumbi yaweza kusababisha mtu kupiga chafya, baridi au moshi vinaweza kumfanya mtu kukohoa, kula baadhi ya vitu vinaweza kumfanya mtu kupata maradhi ya ngozi, kunusa au kupata harufu ya baadhi ya mafuta mazuri yanaweza kumfanya mtu aumwe na kichwa n.k. Hali zote hizi ni mifano ya mzio. Tiba kubwa ya mzio ni kuepukana na yale yote yanayosababisha mzio. B. PUMU (ASTHMA):Haya ni maradhi ambayo husibu mapafu na kumsababisha mgonjwa apate shida ya kupumua. SABABU: Yawezekana kusababishwa na vumbi, aina ya unga au vumbi litokanalo na maua, baadhi ya vyakula, mabadiliko ya hali ya hewa, wanyama kama paka na mbwa, aina ya bacteria, kuvuta sigara, pumu ya kurithi. n.k. DALILI: (3) Mgonjwa hupata shida ya kupumua ndani hewa safi ya oksijeni na kupumua nje hewa chafu ya kabondayoksaidi. (4) Wakati mwingine utamsikia mgonjwa akipumua anatoa sauti isiyokua ya kawaida(wheezing sound)hii ni kwa sababu ya wingi wa makohozi (mafua) yaliyosongamana ndani ya mapafu na kuzuia nafasi ya hewa. Mgonjwa hupata shida anapokua ndani ya chumba ambacho ndani yake hakuna hewa ya kutosha kwa sababu ya udogo au upungufu wa madirisha. Mgonjwa hupata nafuu baada ya kutoa na kutema makohozi na kukaa sehemu yenye hewa safi. (5) Kukohoa au kikohozi cha muda mrefu.TIBA: Kanuni ya kwanza: Chukua bakuli yenye maji ya moto kisha udondoshee ndani yake matone kadhaa ya mafuta ya habatsoda. Kaa juu ya kiti halafu ujifunike shuka na usogeze bakuli lenye maji ya moto na habat soda ili upate mvuke wake. Tiba hii inaitwa Aromatherapy. Baada ya kufanya hivyo jipake mafuta ya habat soda mgongoni na kifuani halafu unywe mafuta ya habat soda matone matatu. Tumia kanuni hii kutwa mara mbili asubuhi na jioni kwa muda wa wiki mbili. Kanuni ya pili: Chukua asali nusu lita, juisi ya kitunguu saumu mili lita 200, unga wa habat soda vijiko vinne vikubwa, unga wa tangawizi vijiko viwili vikubwa, unga wa mdalasini kijiko kimoja kikubwa. Vyote changanya pamoja. Kula vijiko viwili vikubwa kutwa mara tatu. C. MAFUA (FLU NA COMMON COLD). HAYA ni maradhi maarufu, ambayo huambukiza kwa urahisi kutoka kwa mgonjwa hadi kwa mtu mwingine. TIBA: Chukua asali robo lita, unga wa tangawizi vijiko viwili vikubwa, unga wa mdalasini kijiko kimoja kikubwa na unga wa habasoda vijiko viwili vikubwa. Changanya zote pamoja kwa kukoroga kwa kijiko. Kula vijiko viwili vikubwa kutwa mara tatu. D. MATATIZO YA MASIKIO:Bila shaka viungo au mishipa ya masikio, pua na koo yameungana na yana uhusiano wa karibu. Kwa hivyo kiungo kimoja kikiathirika yawezekana viungo vingine kuathirika, ikiwa vishambulizi vya bacteria vitasambaa hadi sehemu nyingine. Sikio ni kiungo maalum katika viungo vya hisia ambayo kazi yake ni kusikia. Reply Evarm10:03 1st November 2011 Asante sana mzizi mkavu! Big up mkuu! Reply MziziMkavu00:08 29th November 2011 MATATIZO YA MACHO: KONJACTIVA (CONJUCTIVITS):Ni maradhi ya macho sehemu ya utando au ute sehemu ya conjuctiva, ambayo inaunganisha sehemu ya ndani ya jicho na kope. SABABU: Yanaweza kusababishwa na vumbi, moshi, upepo ulio na ubaridi, kuweza kutumia macho kwa muda mrefu kutizama kwa mfano kusoma, kukaa katika mwanga mkali wa jua, upepo wenye ukavu na ujoto wenye hali ya umoto, mvuke, gesi, moto, kemikali, n.k. DALILI: Kujikuna, kuvimba macho, macho kuwa mekundu, macho kutoa maji au machozi, kuhisi kuna mchanga ndani ya macho, kuogopa mwanga mkali, n.k. TIBA: Weka macho yawe safi na uyakoshe kwa maji ya baridi. Epusha macho kutokana na joto, baridi, moshi, vumbi, macho yasitumie nguvu sana kama vile kusoma sana. Tumia dawa za kulainisha choo ikiwa hupati choo vizuri kwa sababu pia huchangia katika maumivu ya kichwa na macho. MARADHI YA KUTOPATA CHOO (CONSTIPATION): Haya ni maradhi ambayo mgonjwa huwa hapati choo kwa wepesi. Haja kubwa inaweza kutoka baada ya siku moja au mbili au zaidi na ikitoka huwa ni kigumu na hutoka kwa shida na wakati mwingine huwa kama cha mbuzi. Wagonjwa wengine hupata maumivu wakati wa kwenda haja kubwa. Mtu mwenye afya nzuri hupata haja kubwa kwa kiwango cha chini mara moja kwa siku. Na choo huwa laini na hutoka bila matatizo. SABABU ZA MARADHI HUSIKA: (1) Upungufu wa vitamini mwilini hasa vitamin B. (2) Maradhi ndani ya utumbo mpana. (3) Kula vitu vigumu na vikavu kama vile vyakula vya ngano. (4) Upungufu wa ulaji matunda na mboga. (5) Kutokunywa
NAIPENDA NCHI YANGU TANZANIA;
TANZANIA IS BEAUTIFUL COUNTRY! Have a look at wild life
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, 31 OKTOBA 2005
TAFAKARI Mke kanunua line ya airtel amsurprise mumewe, Mume amekaa sitting room, mke akaenda jikoni akampigia mume na number mpya akasema \"HALLO DARLING\", Mume hakuijua number akajibu kwa sauti ya chini \"KATA NTAKUPIGIA...! Mke wangu yuko jikoni atasikia!...................... Tafakari nini kitaendelea?
Jokes: Humor, Jokes and Funny Pictures
ANGALIA CARTOON NZURI KWA YOUTUBE HAPA.
SEARCH YOUR VIDEO
MY ALBUM